Matthew 23:29-32

29 a“Ole wenu, walimu wa sheria na Mafarisayo, ninyi wanafiki! Mnajenga makaburi ya manabii na kuyapamba makaburi ya wenye haki. 30Nanyi mwasema, ‘Kama tungaliishi wakati wa baba zetu, tusingalikuwa tumeshiriki katika kumwaga damu ya manabii!’ 31 bHivyo mnajishuhudia wenyewe kwamba ninyi ni wana wa wale waliowaua manabii. 32 cHaya basi, kijazeni kipimo cha dhambi ya baba zenu!

Copyright information for SwhKC